Watumishi wa afya DRC wagoma huku maambukizi ya Ebola yakiongezeka

Takriban watumishi wa afya 100 wanasema kutolipwa marupurupu yao kunawakatisha tamaa.

Newstimehub

Newstimehub

26 Julai, 2026

17f6e5ea 6a29 4b5f 85ae 26c29d47bcda 1784983975871

Wafanyakazi wa afya katika kituo cha matibabu ya Ebola mashariki mwa Congo wamefanya mgomo siku ya Jumamosi kufuatia tatizo la malipo, na kusababisha huduma kusita wakati ambapo nchi hiyo inakabiliana na mlipuko wa ugonjwa huo.

Idadi ya maambukizi ya Ebola yaliyothibitishwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imefikia 2,973, ikiwemo vifo 1,309, kwa mujibu wa takwimu za serikali zilizotolewa Ijumaa ambapo serikali inasema ni mlipuko ulioweka rekodi ya kuenea kwa kasi.

Shughuli zote zilikwama katika Kituo cha Kutoa Matibabu ya Ebola cha Elikya kilichopo Bunia, mkoa wa Ituri, hii ni baada ya madaktari, wauguzi na walinzi kugoma kufanya kazi.

Takriban wafanyakazi wa afya mia moja waliandamana nje ya kituo siku ya Jumamosi.

Walisema kutolipwa kwa marupurupu kunakatisha tamaa na kutatiza huduma kwa wagonjwa, hivyo kuitaka serikali kulipa stahiki zao ili warudi kazini.