Wafungwa wasiopungua 50 walitoroka kutoka gereza moja katika jimbo la Kasai nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, maafisa walisema mwishoni mwa siku ya Jumamosi.
Msimamizi wa eneo hilo, Jean Tshiawuke wa Tshiawuke, alisema wafungwa hao walivunja njia na kutoka katika gereza la Luebo, lililoko kusini-kati mwa nchi hiyo, usiku wa kuamkia Ijumaa.
“Gereza lote lilibaki tupu. Ilikuwa ni jaribio la kutoroka lililopangwa vyema, kwani wafungwa hawakuvunja kufuli,” Tshiawuke aliwaambia waandishi wa habari.
Alisema maafisa wa usalama wanashukiwa kuhusika katika tukio hilo , jambo lililowawezesha wafungwa wote kuondoka gerezani.
Bunduki zimepotea
Afisa huyo alionyesha wasiwasi kuhusu athari za kiusalama za tukio hilo, akisema kuwa miongoni mwa waliotoroka kulikuwa na wafungwa waliochukuliwa kuwa hatari kwa jamii.
Tshiawuke alisema operesheni ya kuwatafuta imeanzishwa na kwamba bunduki tatu pia zilichukuliwa wakati wa tukio hilo la kutoroka.
Aliwasihi wakazi kuripoti iwapo watawaona wafungwa hao waliotoroka katika eneo hilo na kusaidia mamlaka kuwakamata tena.















