Burkina Faso, Mali na Niger zimeanza rasmi mchakato wa kujiondoa ICC

Burkina Faso, Mali, na Niger zimeanzisha mchakato wa kujiondoa katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), mahakama hiyo imesema katika taarifa.

Newstimehub

Newstimehub

2 Julai, 2026

c9f115dc8b5caa1443c76421ff51ad426e9fbfce885d1e8a4edb8962664dab02 main

Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imethibitisha kuwa Burkina Faso, Mali na Niger zimewasilisha rasmi notisi za kujiondoa katika mahakama hiyo, hatua iliyoanzisha mchakato wa mwaka mmoja wa kujiondoa kwenye Mkataba wa Roma ulioanzisha ICC.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ICC, nchi hizo tatu za Afrika Magharibi zilitangaza mwezi Septemba 2025 kuwa zitaondoka katika mahakama hiyo, zikiituhumu kuwa ni “chombo cha ukandamizaji wa ukoloni mamboleo.”

ICC ni mahakama ya kimataifa inayoshughulikia kesi dhidi ya watu wanaotuhumiwa kwa mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya ubinadamu, uhalifu wa kivita, pale ambapo mahakama za kitaifa zinashindwa au haziwezi kuchukua hatua.

Katika taarifa iliyochapishwa Jumatano, uongozi wa chombo kinachosimamia ICC ulithibitisha kupokea barua za kujiondoa kutoka Mali, Burkina Faso na Niger, hatua inayozindua rasmi kipindi cha mwaka mmoja kabla ya kujiondoa kwao kukamilika.