Benin yawakamata watu karibu 30 kuhusiana na jaribio la mapinduzi

Benin imewakamata watu takriban 30, wengi wao wanajeshi, kwa madai ya kuhusika na jaribio la mapinduzi lililotibuliwa mwezi huu, vyanzo vya kisheria vimeiambia AFP.

Newstimehub

Newstimehub

16 Desemba, 2025

c6d7b92717451588a610f4781e56138c6d16759214d3d4918eda2256d05b9687

Benin imewakamata watu karibu 30, wengi wao wakiwa wanajeshi, kwa madai ya kuhusika na jaribio la mapinduzi lililotibuliwa mwezi huu, vyanzo vya kisheria vimeiambia AFP.

Wanajeshi walijitokeza kwenye televisheni ya taifa Disemba 7 kutangaza kuwa Rais Patrice Talon amepinduliwa lakini jaribio hilo la mapinduzi lilitibuliwa na wanajeshi watiifu.

Watu kadhaa waliuawa na kiongozi wa yaliyodaiwa kuwa mapinduzi, Luteni Kanali Pascal Tigri, na wanajeshi walioasi hawajulikani waliko.

Siku ya Jumatatu, watu karibu 30 wanaoshtumiwa walifikishwa mbele ya mwendesha mashtaka maalum wa mahakama ya uhalifu wa kiuchumi na ugaidi katika mji wa Cotonou, vyanzo vilisema siku ya Jumanne.

Kukamatwa kabla ya kesi

Walizuiwa kabla ya kesi siku ya pili baada ya shauri lao kusikilizwa, waliongeza.

Wanashtakiwa na “uhaini”, “mauaji” na “kuhatarisha usalama wa nchi”, vyanzo hivyo vilisema.

Kulikuwa na ulinzi mkali katika maeneo ya mahakamani, mwandishi wa habari wa AFP alishuhudia.

Kwingineko, Chabi Yayi, mtoto wa kiume wa rais wa zamani wa Benin na mwanasiasa wa upinzani sasa hivi Thomas Boni Yayi, aliachiliwa huru siku ya Jumatatu baada ya kuhojiwa siku ya Jumatatu.