Wizara ya Ulinzi ya Marekani yaishiwa na fedha

Inadaiwa kuwa, kushindwa kufikiwa kwa sitisho la kumaliza vita dhidi ya Iran, kutaongeza gharama zaidi kwa wizara hiyo.

Newstimehub

Newstimehub

21 Julai, 2026

9e9421ff fe30 4162 80fd f4e4623f8cd4 1784656967538

Wizara ya Ulinzi ya Marekani, maarufu kama Pentagon, inakabiliwa na uhaba mkubwa wa fedha, kutokana na taifa hilo kuendelea kupigana na Iran.

Likiwanukuu maofisa wa Marekani siku ya Jumanne, jarida la The Washington Post limesema kuwa uhaba huo wa fedha, umelilazimu jeshi la Marekani kupunguza mazoezi na matengenezo ya vifaa vya kijeshi.

Inadaiwa kuwa, kushindwa kufikiwa kwa sitisho la kumaliza vita dhidi ya Iran, kutaongeza gharama zaidi kwa wizara hiyo.

Hayo yanajiri wakati Ikulu ya White House nchini Marekani, ikiomba kuidhinishiwa Dola bilioni 67, kama mfuko wa dharura, japo haijapitishwa bado na bunge la Congress.