Moto wazuka karibu na kiwanda cha kusafisha mafuta Libya baada ya mashambulizi

Mashambulizi hayo yalisababisha kukatika kwa umeme na kusababisha ukosefu wa umeme kusini mwa mji wa Zawiya.

Newstimehub

Newstimehub

12 Agosti, 2026

9f0373cd 887b 430a b9a9 914cecdab1fe 1786523867392

Shirika la Umeme la Libya siku ya Jumatano lilisema mashambulizi katika kituo cha kufua umeme cha Zawiya Kusini yamesababisha kukatika kwa umeme na kukosekana kwa umeme kote kusini mwa mji wa Zawiya.

Picha za video katika vyombo vya habari vya Libya zilionesha moto ukiwaka kutoka kwenye kituo cha umeme kufuatia taarifa za mashambulizi.

Kampuni hiyo iliongeza kuwa mashambulizi ya mara kwa mara yamesababisha uharibifu mkubwa katika kituo cha kufua umeme cha Zawiya, kulazimisha shirika hilo kuondoa wafanyakazi wake wa idara ya ufundi, na huenda ikasababisha kucheleweshwa kwa ukarabati na kurudishwa kwa huduma za umeme.

Shambulizi hilo limefuatia mashambulizi ya ndege zisizokuwa na rubani katika mapipa ya kuhifadhi mafuta eneo la karibu la Zawiya, ambalo lina kiwanda kikubwa cha kusafisha mafuta.

Kuanza tena kwa vurugu katika mji wa kimkakati wa Libya wa Zawiya kumetatiza sekta ya mafuta katika nchi hiyo wanachama wa OPEC, huku Shirika la Mafuta la Taifa likisema kuwa litatangaza hali ya dharura kama mashambulizi ya ndege zisizokuwa na rubani yataendelea kwa miundombinu ya nishati katika mji huo.