Msemaji wa klabu ya Young Africans ya nchini Tanzania, Ali Kamwe, amesisitiza umoja ndani ya klabu hiyo, inapojiandaa na mchezo wa wake dhidi ya Azam FC katika Ligi Kuu ya NBC.
Kulingana na Kamwe, lengo kubwa ni kuhakikisha timu hiyo inamaliza msimu kwa mafanikio na kutetea ubingwa wake.
Aliongeza kuwa, kila mchezo uliobaki una umuhimu mkubwa kwa Yanga na hakuna nafasi ya kufanya makosa, kwani kupoteza pointi katika hatua hii ya mwisho kunaweza kuathiri malengo yao ya kutwaa taji la ligi.
“Tunatakiwa kushikamana kuhakikisha tunafanya vizuri katika michezo hii iliyosalia. Tutaumia sana tukiangusha pointi na kupoteza ubingwa,” amesema Kamwe.
Young Africans itamenyana na Azam FC, Juni 24, 2026 katika uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.















