Athari za vita inayohusisha Iran zinaendelea kusambaa katika uchumi wa dunia, hasa katika sekta ya chakula na kilimo.
Athari za vita inayohusisha Iran zinaendelea kusambaa katika uchumi wa dunia, hasa katika sekta ya chakula na kilimo.
Ripoti zinaonyesha kuwa usambazaji wa mbolea umeathirika vibaya kutokana na kuzuiwa kwa njia muhimu za biashara, jambo linalopunguza uzalishaji wa mazao.
Mkurugenzi wa kampuni ya mbolea ameonya kuwa hali hiyo inaweza kusababisha kupungua kwa uzalishaji wa chakula kwa kiwango kikubwa, na kuweka mabilioni ya milo katika hatari.
Aidha, kupanda kwa gharama za mbolea, mafuta na usafirishaji kunazidi kuongeza mzigo kwa wakulima, hali inayoweza kusababisha kupanda kwa bei ya vyakula duniani.
Mashirika ya kimataifa yanaonya kuwa ikiwa hali itaendelea, inaweza kuathiri zaidi nchi maskini na kuongeza idadi ya watu wanaokabiliwa na njaa.
Chanzo:Newstimetr














