Soko la Gikomba linatajwa kuwa moja ya masoko makubwa zaidi ya wazi Afrika Mashariki, likihudumia zaidi ya wafanyabiashara na wafanyakazi 100,000.
Soko hilo ni kitovu muhimu cha biashara ya mitumba, viatu na bidhaa mbalimbali, na huchangia kwa kiasi kikubwa uchumi wa kila siku wa Nairobi pamoja na nchi jirani kama Uganda, Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Hata hivyo, ubomoaji wa hivi karibuni umeathiri shughuli hizo, huku maelfu ya watu wakipoteza chanzo chao cha mapato.
Serikali imeeleza kuwa ina mpango wa kujenga soko la kisasa lenye thamani ya takribani dola milioni 40, ambapo wafanyabiashara watahamishiwa. Lakini hadi sasa, wengi wao wanaendelea kuishi katika hali ya sintofahamu wakisubiri hatua zaidi.
CHANZO: Newstimetr












