Wataalamu wa sekta ya madini wanaonya juu ya uwezekano wa uhaba wa madini ya kobalti na shaba kutokana na kucheleweshwa kwa usafirishaji.
Mshauri wa masuala ya madini, Isabel Ramirez, amesema kuwa muda wa kusafirisha mizigo umeongezeka kutoka miezi mitatu hadi kufikia miezi sita.
Amesema mabadiliko ya njia za meli na kupungua kwa mizigo kunachangia hali hiyo, ambayo inaweza kuathiri upatikanaji wa malighafi muhimu kwa magari ya umeme na nishati safi duniani.
CHANZO: Newstimetr











