Katika mwendelezo wa sera za uongozi wa Denis Sassou Nguesso, serikali mpya inayotarajiwa kuundwa na Anatole Collinet Makosso inatarajiwa kuweka mkazo mkubwa kwenye uchumi na ajira kwa vijana.
Republic of Congo, ambayo ina watu takriban milioni 6, inategemea sana sekta ya mafuta, inayochangia karibu asilimia 80 ya mapato ya mauzo ya nje.
Kutokana na hali hiyo, serikali imeweka mpango wa kuimarisha sekta nyingine kama kilimo cha kisasa na viwanda ili kupunguza utegemezi huo.
Hatua hii inalenga kuunda ajira zaidi, hasa kwa vijana, na kuimarisha uchumi wa taifa kwa muda mrefu.
CHANZO: Newstimetr














