Marekani yaondoa dhamana ya viza ya Dola 15,000 kwa mashabiki kutoka nchi tano za Afrika

Mataifa matano ya Afrika ambayo yamefuzu kwa fainali za Kombe la Dunia ni miongoni mwa nchi ambazo raia wake wanatakiwa kulipa dhamana ya viza: Algeria, Cape Verde, Ivory Coast, Senegal na Tunisia.

Newstimehub

Newstimehub

14 Mei, 2026

72c816934bad6f1580871ef65dc48885831c6a59ac8aa1e98a1b698d4adc3526

Marekani imesema siku ya Jumatano kuwa itarahisisha masharti yake ya malipo ya dhamana kwa baadhi ya mashabiki wanaoomba viza ya kwenda kutizama fainali za Kombe la Dunia.

Ikiwa ni moja ya mipango ya Rais Donald Trump kukabiliana na uhamiaji, Marekani ilianza kutaka dhamana ya kuomba viza ya Marekani kwa raia kutoka mataifa 50 ya kati ya Dola 5,000 hadi 15,000, ambazo zinarudishwa pindi mtu anaporudi nyumbani.

Wizara ya Mambo ya Nje inasema itaondoa dhamana ya viza kwa timu zinazoshiriki kwenye Kombe la Dunia pamoja na mashabiki wake ambao wana tiketi tayari na wameomba huduma ya haraka ya kupata viza.

Mataifa matano ya Afrika ambayo yamefuzu kwa fainali za Kombe la Dunia ni miongoni mwa nchi ambazo raia wake wanatakiwa kulipa dhamana ya viza: Algeria, Cape Verde, Ivory Coast, Senegal na Tunisia.

“Bado tumedhamiria kuimarisha usalama wa Marekani huku tukifanya iwe rahisi kwa wale wasafiri wenye nia njema kwa ajili ya Kombe la Dunia,” alisema Mora Namdar, naibu waziri wa mambo ya nje anayeshughulikia masuala ya huduma za ubalozi.

‘Kombe la Dunia la FIFA bora zaidi’

Alisema serikali ya Trump ilitaka kuandaa “mashindano makubwa na bora zaidi ya kombe la Dunia la FIFA katika historia.”

“Tangazo la leo kutoka kwa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani linadhihirisha kuwa ushirikiano wetu unaoendelea pamoja na serikali ya Marekani na Kikosi Kazi cha Ikulu ya White House kuhusu Kombe la Dunia la FIFA kuwa na michuano yenye mafanikio, ya kihistoria na ambayo hayatosahauliwa daima,” msemaji wa FIFA alisema katika taarifa.

Serikali ya Trump pia iliongeza ufuatiliaji kwa raia wanaotoka nchi marafiki za Magharibi, ikitaka iruhusu serikali ya Marekani kufanya uchunguzi wa akaunti zao za mitandao ya kijamii.

Kombe la Dunia, ambalo linaanza Juni 11, litafanyika nchini Canada, Mexico na Marekani.