Chama cha soka cha Palestina chaituhumu FIFA kwa kushindwa kuiadhibu Israel

Chama hicho, kimeikosoa FIFA kwa kuendelea kukaa kimya na kutochukua hatua dhidi ya vitendo vya Israel dhidi ya Palestina.

Newstimehub

Newstimehub

4 Agosti, 2026

2fda4878 d03e 4529 8e0d 5bb97d367557 1785826140178

Chama cha soka cha Palestina (PFA) kimedai kuwa Shirikisho la Soka Ulimwenguni (FIFA) lilishindwa kutumia baadhi ya sheria zake dhidi ya Israel kwa matendo yake yanayoendelea kuathiri ustawi wa mchezo wa soka nchini Palestina.

Katika taarifa yake ya Jumatatu, PFA ilidai kuwa zaidi ya watu 1000, wanaojihusisha na mchezo huo nchini Palestina, wameuawa katika eneo la Gaza, huku viwanja vya michezo na maeneo mengine yakiharibiwa vibaya.

Chama hicho, kimeikosoa FIFA kwa kuendelea kukaa kimya na kutochukua hatua dhidi ya vitendo vya Israel dhidi ya Palestina.

“Ukimya huu hauridhishi hata kidogo, hatuwezi kuendelea kusikiliza ahadi zisizotimizwa.”

Mwaka jana, FIFA ilisema haitoifungia Israel kushiriki michezo ya kimataifa, kwani haihusiki na changamoto za kisiasa.

Mashabiki wa soka, wameikosoa FIFA kwa upendeleo, kwa kushindwa kuiadhibu Israel, wakati ilifanya hivyo kwa Urusi kufuatia vita vya Ukraine.