Mahakama nchini Syria siku ya Jumanne ilimhukumu kifo Rais wa zamani wa nchi hiyo Bashar al Assad ambaye hakuwepo mahakamani kwa kupanga mauaji, mateso, kufunga watu bila hatia na uhalifu dhidi ya ubinadamu, shirika la habari la SANA liliripoti.
Jaji Al Aryan wa Mahakama ya jijini Damascus anasema ushahidi uliotolewa umebaini kuhusika kwa Assad katika uhalifu huo kama “aliyekuwa na jukumu la juu zaidi,” na kwamba alitumia taasisi za dola kutekeleza mipango hiyo.
Mahakama hiyo ilimhukumu Assad kwa kupanga mauaji ya watu kadhaa, ikiwemo watoto, mateso, kufunga watu wasiokuwa na hatia na uhalifu dhidi ya ubinadamu, na kumhukumu kifo licha ya yeye kutokuwepo mahakamani.















