Rais wa Senegal Faye ‘anashughulikia mwenyewe’ mazungumzo kuhusu deni na IMF

Rais Bassirou Diomaye Faye amekutana na mkuu wa IMF Kristalina Georgieva pembeni mwa kongamano la nchini Kenya, na wawili hao walijadili uwezekano wa kutatua tatizo la madeni ya Senegal.

Newstimehub

Newstimehub

13 Mei, 2026

ed6c39f822d198e9ed8cdd28eff34692b8f4c85fba7693305875e5e5f8d0cfdc

Rais wa Senegal Bassirou Diomaye Faye yeye mwenyewe anashughulikia mazungumzo na Shirika la fedha duniani, IMF yenye lengo la kutatua matatizo ya madeni, ofisi yake ilisema siku ya Jumanne kupitia mtandao wa kijamii.

Faye alikutana na mkuu wa IMF Kristalina Georgieva pembeni mwa Kongamano la Afrika jijini Nairobi, na wawili hao walijadili uwezekano wa kutatua tatizo la madeni ya Senegal.

IMF ilisitisha mradi wa dola bilioni $1.8 2024 baada ya taarifa za kutatanisha kuibuka awali.

Taifa hilo la Afrika Magharibi linataka kukopa ili kukabiliana na mzigo wake wa madeni.

Faye na Georgieva wamekubaliana kuendelea na majadiliano, ofisi ya Faye ilisema.

‘Yeye mwenyewe amedhamiria’

“Hili ni suala ambalo Rais mwenyewe amedhamiria kukabiliana nalo na amejitolea kwa dhati kabisa katika hili,” ilisema.

Waziri Mkuu Ousmane Sonko mwaka uliopita alisema IMF ilitaka Senegal kuja na mpangilio wa deni lake na serikali itapinga hatua kama hiyo, ikiitaja kuwa “ya aibu”.

Faye na Georgieva pia walijadili namna ya kukabiliana na suala la uchumi kutokana na vita vya Mashariki ya Kati, “hasa kupanda kwa gharama za nishati na athari zake kwa uchumi wa nchi,” Ofisi ya Faye ilisema.