Baada ya Turkish Airlines kutangaza kurejesha safari zake kuelekea Damascus, Beirut na Amman, wachambuzi wa sekta ya anga wanaamini mashirika mengine ya kimataifa yanaweza kufuata mkondo huo iwapo hali ya usalama itaendelea kuimarika katika Mashariki ya Kati.
Wataalamu wanasema mara nyingi mashirika makubwa ya ndege hutumika kama kipimo cha kuaminika kuhusu tathmini ya usalama wa anga katika maeneo yenye changamoto za kisiasa au kijeshi.
Iwapo kurejea kwa safari hizo kutafanikiwa bila changamoto, mashirika mengine yanaweza pia kutangaza kurejesha huduma zao katika miezi ijayo, jambo litakaloongeza ushindani na kupunguza gharama za usafiri kwa abiria.
Hatua hiyo pia inaweza kusaidia kufufua sekta ya anga katika eneo hilo ambalo limeathiriwa kwa kiasi kikubwa na taharuki za kiusalama katika miezi ya karibuni.
CHANZO: Newstimetr














