Mvutano wa kidiplomasia umeibuka kati ya Madagascar na Ufaransa baada ya serikali ya Madagascar kumtaka afisa mmoja wa ujasusi katika ubalozi wa Ufaransa kuondoka nchini.
Hatua hiyo imechukuliwa kufuatia uchunguzi wa madai ya njama za kisiasa zinazomhusisha mwanajeshi wa zamani wa Ufaransa na washirika wake.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Madagascar imesema afisa huyo alijihusisha na shughuli zisizoendana na hadhi yake ya kidiplomasia, ingawa haikufichua jina lake wala maelezo zaidi.
Tukio hilo linaashiria kuongezeka kwa mvutano kati ya Antananarivo na Paris wakati uchunguzi kuhusu madai ya njama ya mapinduzi ukiendelea.
CHANZO: Newstimetr














