Wachambuzi wa usalama wameonya kuwa kurejea kwa vitendo vya uharamia katika pwani ya Somalia kunaweza kusababisha usumbufu mkubwa kwa biashara ya baharini duniani.
Onyo hilo limefuatia tukio la hivi karibuni la kutekwa kwa meli ya mizigo pamoja na taarifa za kuongezeka kwa shughuli za makundi ya maharamia katika eneo la Somali Basin.
Wataalamu wanasema hali hiyo inajitokeza wakati njia nyingine muhimu za biashara duniani tayari ziko kwenye presha kutokana na mvutano katika Mlango wa Hormuz, jambo linaloongeza hatari kwa sekta ya usafiri wa kimataifa.
Ikiwa mashambulizi yataongezeka, gharama za usafirishaji na bima ya meli zinaweza kupanda kwa kiasi kikubwa, hali ambayo inaweza kuathiri uchumi wa kimataifa.
CHANZO: Newstimetr














