Hali ya usalama katika Sudan Kusini inaendelea kuzorota baada ya mapigano mapya kusababisha wakazi wa Akobo kukimbia makazi yao kwa wingi.
Kwa mujibu wa UNICEF, takriban watu 100,000 wamekimbilia Ethiopia, huku wengine wakisambaa katika maeneo ya ndani kama Upper Nile.
Ripoti zinaonyesha kuwa hospitali na vituo 28 vya afya vimeharibiwa au kufungwa, wakati mlipuko wa kipindupindu ukiendelea katika eneo hilo.
Mgogoro huo unahusishwa na kuvunjika kwa makubaliano ya kugawana madaraka kati ya Salva Kiir na mpinzani wake Riek Machar.
CHANZO: Newstimetr














