Tatizo la uchimbaji haramu wa madini limeendelea kuongezeka katika maeneo ya migodi iliyotelekezwa karibu na Johannesburg.
Kwa mujibu wa mamlaka, kuna zaidi ya mashimo ya migodi 6,000 yaliyotelekezwa nchini humo, ambayo yamekuwa yakivamiwa na wachimbaji haramu wanaojulikana kama “zama zamas”.
Wachimbaji hao huingia kwenye migodi hiyo kutafuta mabaki ya dhahabu au madini mengine yenye thamani, mara nyingi wakifanya kazi katika mazingira hatari bila kibali cha serikali.
Biashara hiyo pia inaaminika kuhusisha mitandao ya uhalifu yenye silaha na wahamiaji kutoka nchi jirani kama Lesotho, Zimbabwe na Mozambique.
CHANZO: Newstimetr














