Rwanda kubadilisha sheria ya matumizi ya barabara

Sheria iliyopo ya barabarani, iliyotungwa mwaka 1987, inaonekana kama imepitwa na wakati hivyo haiendani na hali halisi ya matumizi ya sasa ya barabara, kwa mujibu wa maelezo yanayoambatana na muswada huo mpya.

Newstimehub

Newstimehub

10 Septemba, 2025

2025 05 15t094411z 1 lynxmpel4e0fy rtroptp 3 migration britain rwanda

Serikali ya Rwanda imewasilisha rasimu ya sheria mpya inayosimamia usalama wa barabarani mbele ya Bunge ili kurekebisha sheria ya sasa ya barabarani nchini, ambayo haijabadilishwa kwa takriban miongo minne.

Sheria iliyopo ya barabarani, iliyotungwa mwaka 1987, sasa inaonekana kupitwa na wakati na kutoendana na hali halisi ya matumizi ya kisasa ya barabara, hayo ni kwa mujibu wa maelezo yanayoambatana na mswada huo mpya.

Kikao cha Baraza la chini la Bunge kilipitisha umuhimu wa mswada huo, ambao utachambuliwa na Kamati ya Bunge inayowajibika kabla ya kupigiwa kura.

“Mapitio ya sheria iliyopo muhimu ili kuhakikisha usalama barabarani, kukabiliana na teknolojia zinazobadilika na tabia za udereva, na kudumisha ufanisi wa sheria za trafiki, na hatimaye kulenga kupunguza ajali na majeruhi,” alisema Waziri wa Miundombinu, Jimmy Gasore.

Alisema marekebisho hayo yamechelewa, kwani sheria ya mwaka 1987 haishughulikii ipasavyo changamoto za sasa katika usimamizi wa matumizi ya barabara.

Ingawa inadhibiti matumizi ya barabara za umma – ikiwa ni pamoja na watu, wanyama, na magari – sheria inatekelezwa kupitia vyombo kadhaa, ikiwa ni pamoja na Amri ya Rais ya 2002 (pamoja na marekebisho mwaka wa 2005, 2008, na 2015); agizo la mawaziri la 2024 juu ya modeli ya leseni za kitaifa za kuendesha; na agizo la mawaziri la 2020 linaloweka ada ya juu zaidi ya ukaguzi wa kiufundi wa gari.