Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio kukutana na Papa Leo XIV

Mazungumzo hayo yanakuja wakati kukiwa na mvutano wa wazi kati ya Ikulu ya Vatican na Makao Makuu ya Kanisa Katoliki duniani.

Newstimehub

Newstimehub

7 Mei, 2026

166c89f563f6235af63bb8a51880f86a774612f8dc6326997ef86ba0b0b63390

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio, amefika mjini Roma, Vatican kwa ajili ya kikao na Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Leo XIV.

Mazungumzo hayo yanakuja wakati kukiwa na mvutano wa wazi kati ya Ikulu ya Vatican na Makao Makuu ya Kanisa Katoliki duniani.

Ziara hiyo, pia inakuja baada ya Rais Donald Trump wa Marekani, kukosoa waziwazi msimamo wa Papa Leo XIV, kuhusu vita.

Hata hivyo, Rubio ambaye ni muumini wa dhehebu la Kikatoliki, amepuuzia madai ya uhasama kati ya pande hizo mbili, kabla ya ziara hiyo ambayo pia itahusisha mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin.

Ziara hiyo, imeratibiwa na Ikulu ya Marekani, kulingana na Kardinali Parolin.