Rais wa Marekani Donald Trump amesema hataogopa wala kubadili ratiba yake ya kisiasa baada ya kunusurika jaribio la tatu la kuuawa ndani ya miaka miwili.
Akizungumza katika mahojiano na CBS, Trump alisema kuwa anaelewa anaishi katika “ulimwengu wa ajabu” lakini bado yuko tayari kuendelea na majukumu yake kama kawaida.
Kauli yake imekuja wakati mamlaka za usalama zikiendelea na uchunguzi dhidi ya mshukiwa Cole Allen aliyekamatwa baada ya kurushiana risasi na walinda usalama.
Wachambuzi wa kisiasa wanasema msimamo wa Trump unaweza kuongeza taswira yake kama kiongozi mwenye uthabiti mbele ya vitisho vinavyozidi kuikumba siasa ya Marekani.
CHANZO: Newstimetr














