Eneo hilo linalotaka kutambuliwa kimataifa lasema liko tayari kushirikiana na Marekani na Israel katika rasilimali na usalama.
Eneo la Somaliland, linalojitenga na Somalia na kuendelea kutafuta kutambuliwa kimataifa, limesema liko tayari kuipa Marekani ufikiaji wa rasilimali zake za madini na hata vituo vya kijeshi.
Kauli hiyo ilitolewa siku ya Jumamosi, huku Somaliland ikisisitiza kuwa inatafuta washirika wa kimataifa watakaoweza kuwekeza na kushirikiana nayo kiuchumi na kiusalama. Tangu mwaka 1991 ilipojitangaza kujitawala, Somaliland haijatambuliwa rasmi na jumuiya ya kimataifa, isipokuwa Israel ambayo ilitangaza kuitambua mwezi Desemba.
Chanzo: Africanews














