Kashfa ya kuondolewa kwa rasimu ya sera ya taifa ya AI nchini Afrika Kusini imeibua wasiwasi kuhusu kuchelewa kwa mipango ya nchi hiyo kuwa kitovu cha maendeleo ya akili bandia barani Afrika.
Rasimu hiyo ilikuwa imelenga kuiweka Afrika Kusini mbele katika ubunifu wa AI huku ikipendekeza kuundwa kwa taasisi mpya kama Tume ya Taifa ya AI, Bodi ya Maadili ya AI na Mamlaka ya Udhibiti wa AI.
Pia ilikuwa inapendekeza motisha mbalimbali ikiwemo punguzo la kodi, ruzuku na misaada ya kifedha ili kuvutia ushirikiano wa sekta binafsi.
Hata hivyo, baada ya kuondolewa kwa rasimu hiyo, serikali haijatangaza ni lini toleo jipya litawasilishwa.
Wachambuzi wanasema kuchelewa huku kunaweza kuathiri kasi ya Afrika Kusini katika mbio za ushindani wa teknolojia ya AI barani Afrika.
CHANZO: Newstimetr














