Mahakama Kuu ya Kenya: Mchakato wa kumuondoa Gachagua madarakani ulifuata Sheria

Mahakama Kuu ya Kenya imeidhinisha kuondolewa madarakani kwa Gachagua, pamoja na kuamuru kulipwa fidia ya shilingi milioni 50 za Kenya kwa ukiukwaji wa haki zake.

Newstimehub

Newstimehub

8 Juni, 2026

2025 05 15t122810z 611303276 rc26ieaefafc rtrmadp 3 kenya politics

Mahakama Kuu ya Kenya imethibitisha uamuzi wa kumwondoa madarakani aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua, ikiamua kwamba mchakato wa kubanduliwa kwake ulikuwa wa kikatiba na halali.

Katika uamuzi uliotolewa na jopo la majaji watatu, mahakama ilisema Bunge la Kitaifa na Seneti zilifuata mamlaka yao ya kikatiba zilipopitisha uamuzi wa kumwondoa Gachagua madarakani mwaka 2024. Majaji hao waliamua kwamba masharti ya kikatiba ya kuondolewa madarakani kwa Gachagua yalizingatiwa na kwamba uamuzi huo haukuwa batili.

Hata hivyo, mahakama hiyo pia ilibaini kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa baadhi ya haki za kikatiba za Gachagua, hususan haki ya kusikilizwa.

Kutokana na ukiukwaji huo, mahakama ilitoa tamko kwamba haki zake zilivunjwa na ikaamuru apewe fidia ya Shilingi milioni 50 za Kenya.

Majaji hao walisisitiza kuwa ingawa kuondolewa kwake ilikuwa halali na itaendelea kubaki kuwa na nguvu kisheria, ukiukwaji wa haki za kikatiba hauwezi kupuuzwa, hivyo fidia ilitolewa chini ya Katiba ya Kenya.

Gachagua alikuwa amepinga kuondolewa kwake akidai kuwa mchakato huo ulikuwa wa kisiasa, uliokiuka taratibu, na kwamba hakupata nafasi ya kutosha kujitetea. Mahakama ilikataa hoja za kubatilisha kuondolewa kwake madarakani, lakini ikaunga mkono madai ya ukiukwaji wa baadhi ya haki zake.

Mahakama Kuu ya Kenya imethibitisha uamuzi wa kumwondoa madarakani aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua, ikiamua kwamba mchakato wa kubanduliwa kwake ulikuwa wa kikatiba na halali.

Hata hivyo Gachagua bado ana haki ya kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa.