Jeshi la Mali limeonya kuwa makundi yenye silaha bado yanajaribu kuendelea kuweka shinikizo kwa vikosi vya serikali kupitia mbinu za kupenyeza maeneo mapya na kuvuruga njia za usambazaji.
Mkuu wa Majeshi Jenerali Diarra amesema hali ya usalama inaendelea kuimarika katika maeneo mengi yaliyoshambuliwa, lakini vikosi vya usalama vinaendelea na operesheni za kusaka magaidi.
Aidha, amesema jeshi limefanya marekebisho ya kimkakati katika mkoa wa Kidal, ikiwemo kuhamisha baadhi ya vikosi kuelekea Anefis ili kuimarisha udhibiti wa maeneo ya kaskazini.
Katika ujumbe wake kwa wananchi, Diarra amewataka raia kuwa watulivu na kupuuza propaganda pamoja na taarifa za uongo, akisisitiza wananchi kutegemea taarifa rasmi kutoka serikalini pekee.
CHANZO: Newstimetr














