Kiongozi wa vikundi vya silaha katika mashariki mwa Libya, Khalifa Haftar, alituma ujum wa rambirambi Jumanne kufuatia kifo cha Kiongozi wa Jeshi la Libya, Mohammed al-Haddad, na wajumbe waliofuatana naye katika ajali ya ndege karibu na mji mkuu wa Uturuki, Ankara.
Katika taarifa, Haftar ameonyesha hisia za “majonzi makubwa kwa msiba huu wa kusikitisha” na alituma salamu za rambirambi kwa familia ya jenerali aliyefariki na “kwa raia wote wa Libya.”
Vilevile, Bunge la Wawakilishi lililoko Benghazi pia lilituma salamu za rambirambi kwa familia za Haddad na wajumbe waliofuayana naye, pamoja na wenzake katika jeshi.
Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya ilitangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo hivyo.
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki, Ali Yerlikaya, alisema awali kuwa mabaki ya ndege binafsi ya aina ya Falcon 50, iliokuwa ikielekea mjini Tripoli kutoka Uwanja wa Ndege wa Esenboga, Ankara, yalipatikana na vyombo vya usalama vya Uturuki kilomita 2 (1.24 maili) kusini mwa kijiji cha Kesikkavak katika wilaya ya Haymana.








