Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetangaza hatua kali dhidi ya uchimbaji haramu wa madini na vitendo vya ufisadi vinavyohusishwa na sekta hiyo, kufuatia uchunguzi mkubwa ulioanzishwa na Rais Felix Tshisekedi.
Hatua hizo zinajumuisha kukamatwa kwa vifaa vya uchimbaji haramu, kufunguliwa mashitaka ya jinai dhidi ya wahusika, pamoja na kusimamishwa kwa baadhi ya leseni za kampuni zitakazobainika kukiuka sheria.
Rais Tshisekedi amesema hatua hizo ni muhimu ili kurejesha mapato ya taifa na kuhakikisha utajiri wa madini unanufaisha wananchi wa Congo badala ya kupotelea kwa wachache.
Serikali inaamini kuwa mageuzi hayo yataongeza uwazi, kuboresha ukusanyaji wa mapato, na kuimarisha nafasi ya DRC katika soko la kimataifa la madini muhimu kwa teknolojia ya kisasa.
CHANZO: Newstimetr














