Mlipuko wa Ebola DRC wazidi maambukizi 4,000

Wataalamu wanaeleza kuwa hii ni kutokana na kuchelewa kubaini, kuzidiwa katika uchunguzi na mapigano ya kijeshi kama baadhi ya sababu ambazo zimekwamisha juhudi za kukabiliana na ugonjwa huo.

Newstimehub

Newstimehub

7 Agosti, 2026

2cd4c428 2381 450e a197 c4ccf11b6ff4 1786095337074

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imethibitisha kuwa maambukizi ya Ebola yameongezeka zaidi ya 4,000 kwa mara ya kwanza tangu mlipuko huu wa sasa, data za serikali zilionesha.

Ugonjwa huo, umeelezwa kusambaa kwa haraka.

Wataalamu wanaamini huenda maambukizi yalianza kusambaa miezi kadhaa kabla ya mlipuko kutangazwa Mei 15 na idadi ya maambukizi huenda ikawa juu zaidi kuliko ilivyotangazwa rasmi.

Taasisi ya afya ya nchi hiyo ya Afrika ya Kati ilisema katika ripoti yake ya hivi karibuni kuwa idadi ya maambukizi imefika 4,053, ikiwemo vifo 1,850.

Maambukizi kote

Maambukizi yamepatikana katika mikoa mitano ya nchi hiyo:

Ituri, Kivu Kaskazini, Kivu Kusini, Haut-Uele na Tshopo.

Kuchelewa kubaini, kuzidiwa katika uchunguzi, mapigano ya kijeshi, na ukosefu wa chanjo na matibabu ya virusi mahsusi kumefanya iwe vigumu kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa huo.

Kufikia sasa maambukizi ya Afrika Magharibi ya 2014-16 ndiyo makubwa zaidi, kukiwa na maambukizi zaidi ya 28,000 yaliyorekodiwa kote Guinea, Liberia na Sierra Leone.