Awuche wa Ghana, anayeaminika kuwa mtu mrefu zaidi nchini humo, afariki dunia

Sulemana Abdul Samed, anayeaminika kuwa mtu mrefu zaidi nchini Ghana, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 32, shirika la habari la taifa (GBC), limetangaza siku ya Jumatatu.

Newstimehub

Newstimehub

27 Julai, 2026

9a49a004 3ea9 430e a0fe 76e8132604d0 1785175407389

Sulemana Abdul Samed, anayeaminika kuwa mtu mrefu zaidi nchini Ghana, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 32, shirika la habari la taifa (GBC), limetangaza siku ya Jumatatu.

Abdul Samed, kwa jina maarufu Awuche, alifariki wakati akitibiwa katika Hospitali ya Tamale kanda ya kaskazini nchini humo, GBC iliripoti.

Chanzo cha kifo cha Awuche hakikufahamika mara moja.

Alikuwa na urefu wa futi 7 na inchi 4 na mara nyingi alisumbuliwa na changamoto za kiafya kutokana na kimo chake.

Changamoto hizi za kiafya zilimsababishia Awuche kulazwa hospitali mara kwa mara, na mwaka 2022 kukawa na wito wa mchango katika kusaidia kulipa gharama za matibabu yake.

Awuche alisoma shule kaskazini mwa Ghana na baadaye kufanya kazi ya fundi magari.