Serikali ya Nigeria imeongeza juhudi za kidiplomasia kufuatia mvutano unaoendelea dhidi ya wahamiaji nchini Afrika Kusini kwa kumwita Kamishna Mkuu wa Afrika Kusini kwa mashauriano rasmi.
Hatua hiyo imekuja wakati maandamano mapya dhidi ya wahamiaji yakitarajiwa kufanyika kati ya Mei 4 na 8, huku Rais Bola Tinubu akiagiza hali hiyo ifuatiliwe kwa karibu.
Nigeria imesema itaendelea kushirikiana na balozi zake pamoja na mamlaka za Afrika Kusini kuhakikisha usalama wa raia wake unalindwa.
CHANZO: Newstimetr














