Serikali ya Uganda inakabiliwa na shinikizo linaloongezeka baada ya taasisi mbalimbali, ikiwemo Benki ya Dunia, mashirika ya misaada na wanaharakati wa haki, kupinga mswada wa kudhibiti fedha za kigeni.
Wapinzani wa mswada huo wanasema unaweza kuathiri shughuli za maendeleo, kupunguza uwekezaji wa nje na kuhatarisha utulivu wa uchumi wa Uganda.
Benki ya Dunia imeonya kuwa sheria hiyo inaweza kuleta hatari katika utekelezaji wa miradi yake ya maendeleo nchini humo.
Licha ya upinzani huo, serikali ya Uganda imesisitiza kuwa mswada huo una lengo la kulinda uhuru wa taifa na haina madhara kwa uchumi.
CHANZO: Newstimetr














