Ghana imehimiza jumuiya ya kimataifa kupitia United Nations kutambua rasmi biashara ya utumwa ya Atlantiki kama tukio lililobadilisha historia ya dunia na kuanzisha mifumo ya ubaguzi na ukosefu wa usawa.
Kwa mujibu wa maafisa wa Ghana, hatua hiyo haitalenga kupunguza mateso ya matukio mengine ya kihistoria, bali itasaidia kuelewa mizizi ya changamoto za sasa.
Aidha, wameonya kuwa sheria zisitumike kuficha ukweli wa kihistoria, bali ziwe chombo cha haki na uwazi.
CHANZO: Newstimetr














