Kundi la wapiganaji la Palestina Hamas limekubali pendekezo la kusitisha mapigano Gaza kwa siku 60 yaliyowasilisjwa na wapatanishi wa Misri na Qatar, vyombo vya habari vya Misri viliripoti Jumatatu.
Shirika la habari la serikali Al-Qahera News, likitaja vyanzo nchini Misri, linasema kuwa kuna mipango ya kutoa wito kwa vikosi vya Israel kwenda maeneo ya mpakani kusaidia kupitishwa kwa misaada inayoelekea Gaza.
Mapendekezo hayo yanajumuisha kusitishwa kwa muda kwa operesheni za kijeshi kwa miezi miwili, ambapo kipindi hicho kutakuwa na kubadilishana kwa wafungwa, kulingana na taarifa hiyo.
Makubaliano hayo yanazingatia kuachiliwa huru kwa mateka 10 wa Israel walio hai na kurudishwa kwa miili 18, wakibadilishana kwa idadi ambayo haijajulikana ya wafungwa wa Palestina.














