Maelfu wafanya maandamano nchini Sudan kuishukuru Uturuki

Mkutano huo, uliohudhuriwa na maafisa wa Ubalozi wa Uturuki nchini Sudan, ulifanyika katika mji wa Sawakin Jumamosi.

Newstimehub

Newstimehub

10 Agosti, 2025

9875ea5b86fde73701c0f2c9b3dc03fdabac01958bcbceb84606e72d1929ddb6

Maelfu ya watu katika mji wa Sawakin nchini Sudan wamefanya mkutano mkubwa wa hadhara kuonyesha shukrani kwa Uturuki na watu wake kwa msaada wao wakati wa changamoto kubwa nchini Sudan.

Uturuki imekuwa ikisaidia Sudan kwa misaada ya kibinadamu na juhudi za kutatua vita vinavyoendelea nchini humo.

Mkutano huo ulihudhuriwa na maafisa wa Ubalozi wa Uturuki, akiwemo Balozi Fatih Yildiz. Ubalozi wa Uturuki nchini Sudan ulionyesha shukrani kwa mkusanyiko huo wa “Asante Uturuki, Asante Erdoğan”.

Nchi hizi mbili “zitaendelea kusimama pamoja, kama tulivyofanya kwa karne nyingi,” iliongeza katika chapisho kwenye jukwaa la mitandao ya kijamii X.