Marais wa Misri na Iran wajadili juhudi za amani Mashariki ya Kati

Rais wa Misri Abdel Fattah Al Sisi na Rais wa Iran Masoud Pezeshkian wamejadili mazungumzo kati ya Iran na Marekani ya kutaka kufikia makubaliano ya kurudisha amani katika kanda.

Newstimehub

Newstimehub

26 Mei, 2026

8ead306d2e2f35d66dec8ecbd80634dc129229d77eeb2b54c4bab0807fb1492f

Rais wa Misri Abdel Fattah Al Sisi na Rais wa Iran Masoud Pezeshkian wamejadili mazungumzo kati ya Iran na Marekani ya kutaka kufikia makubaliano ya kurudisha amani katika kanda, kulingana na taarifa kutoka ofisi ya rais wa Misri siku ya Jumanne.

Taarifa hiyo inasema kuwa Sisi alipokea simu kutoka kwa Pezeshkian huku mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja kati ya Iran na Marekani yakiendelea na wapatanishi wa kikanda na kimataifa.

Sisi alisisitiza kuhusu msimamo wa Misri kuunga mkono mazungumzo na kueleza kuhusu uhusiano wa kidiplomasia wa Misri na juhudi za kusaidia mazungumzo hayo pamoja na kuelekea kupata “makubaliano ya mwisho na kamili” kwa lengo la kumaliza uhasama na kurudisha usalama.

Rais wa Misri pia alieleza kuhusu mazungumzo yake kwa njia ya simu na Rais wa Marekani Donald Trump na viongozi kadhaa wa Arabuni na katika kanda, akisisitiza kuhusu Misri kuunga mkono kupatikana kwa suluhu ya usalama kwa matatizo ya kikanda.

Fursa ya diplomasia

Taarifa hiyo inasema Sisi alisisitiza “wazi kwa Misri kupinga uchokozi wowote dhidi ya mataifa huru ya Ghuba au vitisho kwa mipaka yao,” huku akieleza umuhimu wa kutoa fursa kwa diplomasia kutumika.

Pezeshkian alieleza kuhusu muelekeo wa majadiliano na kutoa shukrani zake kwa juhudi za Misri na wadau wengine wa kikanda kutatua tofauti kati ya Iran na Marekani.

Rais wa Iran alisisitiza dhamira yake ya kuimarisha uhusiano na mataifa ya Kiarabu, hasa Ushirikiano wa Baraza la Mataifa ya Ghuba, kulingana na taarifa.

Uhasama wa kikanda umeendelea tangu Marekani na Israel walipoanzisha mashambulizi dhidi ya Iran mwishoni mwa mwezi Februari. Iran ililipa kisasi kwa mashambulizi kwa Israel pamoja na washirika wa Marekani katika Ghuba, ikiwa ni pamoja na kufunga Mlango Bahari wa Hormuz.

Kusitishwa mapigano

Mapigano yalisitishwa Aprili 8 kupitia upatanishi wa Pakistan na baadaye Trump akaongeza kipindi cha kusitisha mapigano.

Trump amesema Jumamosi kuwa makubaliano ya kumaliza vita na Iran “yamejadiliwa kwa sehemu kubwa” na anasubiri yakamilike.