Zambia yasitisha zoezi la kuhesabu kura baada ya vurugu

Rais Hichilema katika ujumbe wake kupitia ukurasa wa X amewaomba wananchi “kuwa wavumilivu, na wazalendo.

Newstimehub

Newstimehub

14 Agosti, 2026

ecdee377 f031 4813 b077 da55dc03c068 1786647660852

Tume ya Uchaguzi nchini Zambia imesitisha zoezi la kuhesabu kura Ijumaa na kutoa matangazo ya matokeo nchi nzima baada ya kuwepo kwa taarifa za vurugu zilizolenga maafisa wa Tume katika baadhi ya wilaya.

Maafisa wa Uchaguzi wamesema kumekuwa na matukio ya kuibiwa kwa masanduku ya kupigia kura, na kuongeza kuwa itapitia upya usitishaji huo ndani ya saa 24.

Nchi hiyo ya Kusini mwa Afrika imefanya uchaguzi wa rais, wabunge na viongozi wa serikali za mtaa Alhamisi.

Rais Hakainde Hichilema anagombea muhula wa pili baada ya kupambana na deni la taifa la nchi hiyo tangu kuingia madarakani 2021.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanasema, huenda Hichilema akashinda katika uchaguzi huo, ingawa kiongozi mkuu wa upinzani Brian Mundubile ameonekana kuwa na ushawishi mkubwa katika baadhi ya maeneo.

Matokeo kamili yalitegemewa kutangazwa Jumatatu. Kupitia ukurasa wake wa X, Hichilema amewataka wananchi “kuwa na utulivu, na wazalendo” wanaposubiri matokeo kamili ya uchaguzi.