Maafisa 5 wa usalama wauawa nchini Kenya wakikabiliana na kundi linalodaiwa kuwa la al Shabaab

Kundi la Al-Shabaab limekuwa likifanya vurugu kwa miaka kadhaa likilenga kuipindua serikali kuu ya Somalia.

Newstimehub

Newstimehub

29 Julai, 2026

eaae5c99 c7d8 4aa4 8344 84420eacff73 1785333044351

Maafisa watano wa usalama wameuawa nchini Kenya katika makabiliano na wanaoshukiwa kuwa kundi la kigaidi la Al-Shabaab Kaunti ya Mandera, karibu na mpaka wa Somalia, kwa mujibu wa taarifa ya polisi.

“Maafisa wa kitengo cha operesheni maalum walikabiliana na magaidi wa Al-Shabaab katika eneo la Bwawa la Wantey,” polisi walisema katika taarifa yao kufuatia mapambano siku ya Jumanne majira ya saa sita mchana.

Polisi waliongeza kuwa wanaendelea kuwafuatilia washukiwa hao. Walieleza kuwa kikosi maalum kilichopelekwa eneo hilo kimekumbwa na mlipuko wa bomu la kutegwa ardhini (IED), ambao umeharibu gari la kivita lenye ulinzi maalumu, ingawa hakuna majeruhi walioripotiwa.

Kundi la Al-Shabaab limekuwa likifanya vurugu kwa miaka kadhaa likilenga kuipindua serikali kuu ya Somalia.

Aidha, kundi hilo limekuwa likishambulia mara kwa mara katika eneo hilo, likiwalenga wanajeshi na raia. Polisi walisema kuwa mwezi Januari, kundi hilo limemuuwa chifu wa eneo moja na mwalimu katika Kaunti ya Garissa.