Marekani inatuma matibabu ya majaribio ya Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Uganda huku juhudi za kutengeneza chanjo dhidi ya virusi vya Bundibugyo zikishika kasi.
Mamlaka za afya zinasema zinajitahidi kudhibiti mlipuko huo unasambaa kwa kasi ambao umeambukiza zaidi ya watu 1,200.
Idara ya Afya na Huduma za Kibinadamu ya Marekani ilisema Ijumaa itapeleka kiasi cha matibabu ya majaribio ya antibody MBP134 na vipimo 2,500 vya uchunguzi kusaidia juhudi za majibu katika nchi hizo mbili, ambapo milipuko hiyo imesababisha kuzidiwa mifumo ya afya ya mashinani.
Marekani pia inaunga mkono uundwaji wa chanjo inayolenga hasa aina ya virusi vya Bundibugyo, ambayo kwa sasa hakuna chanjo iliyoidhinishwa.
Hatua za hivi punde zinakuja wakati Taasisi ya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa ya Marekani (CDC) iliinua hatari ya maambukizi kwa Kiwango cha 1 – kiwango chake cha juu cha uanzishaji wa dharura – huku ikidumisha kuwa hatari ya ugonjwa huo kuenea hadi Marekani inabaki chini.
Wakati huo huo Marekani imepokea lawama kuhusu kituo chake cha kudhibiti Ebola nchini Kenya kilichopangwa kuwatibu Wamarekani ambao wameambukizwa virusi hivyo badala ya kuwarudisha nyumbani kwa matibabu.
CDC ilisema zaidi ya watu 1,200 wameambukizwa nchini DRC, na vifo 321 vimeripotiwa, wakati Uganda imethibitisha maambukizi 20.
Mlipuko huo, uliogunduliwa kwa mara ya kwanza mwezi Mei, unasababishwa na aina ya Bundibugyo ya Ebola, mojawapo ya aina zisizo za kawaida za virusi. Tofauti na aina ya Zaire, ambayo chanjo zilizoidhinishwa tayari zipo, hakuna chanjo au matibabu yaliyoidhinishwa mahususi kwa ajili ya Bundibugyo, na kufanya majibu ya sasa kutegemea zaidi hatua za kimatibabu za majaribio.
Shirika la Afya Duniani limependekeza kwamba matibabu ya majaribio na chanjo zitathminiwe kupitia majaribio ya kimatibabu wakati wa mlipuko huo ili kutoa ushahidi juu ya usalama na ufanisi wao huku wakiwapa wagonjwa matibabu yanayoweza kuokoa maisha.















