Marekani yaandaa kituo cha karantini Kenya kwa raia wake walioambukizwa Ebola

Marekani inapanga kuwa na kituo cha karantini Kenya kwa ajili ya raia wake walioambukizwa virusi vya Ebola, gazeti la Wall Street Journal lilitangaza siku ya Jumanne, huku mlipuko hatari ukiongezeka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Newstimehub

Newstimehub

27 Mei, 2026

8df82503fc1f7592d002dd40986b20f4f92a3246bf21a89205ecf6edff538e19

Marekani inapanga kuwa na kituo cha karantini kwa raia wake walioambukizwa Ebola, gazeti la Wall Street Journal liliripoti siku ya Jumanne, huku mlipuko hatari ukiongezeka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Kituo hicho kinatengwa kwa ajili ya Wamarekani ambao watapatikana na virusi vya Ebola au kutagusana na watu waliokuwa wameambukizwa, WSJ lilisema, likinukuu watu walio karibu na suala hilo.

Kituo hicho kitakuwa kwa Wamarekani “ambao watahitaji kuondoka haraka DRC na kukaa katika karantini,” gazeti hilo lilimnukuu afisa mmoja mwandamizi akisema.

Shirika la Afya Duniani limeleza kuwa vifo 10 vimethibitishwa kutokana na Ebola, vifo 220 vinavyoshukiwa na maambukizi 900 yanayodaiwa kuwepo DRC tangu katikati mwa mwezi Mei.

Kituo cha karantini kinasubiri kuidhinishwa na Kenya

Kituo hicho cha karantini kinasubiri kuidhinishwa na mamlaka za Kenya, ambapo hakuna maambukizi yoyote yaliyothibitishwa, WSJ lilisema.

Taarifa hizo zinakuja baada ya daktari mmoja wa Marekani ambaye alikuwa ameambukizwa Ebola wakati akifanya kazi DRC kusafirishwa hadi Ujerumani wiki iliopita.

Hakuna chanjo au tiba kwa virusi hivyo vya aina ya Bundibugyo ambayo imesababisha mlipuko wa 17 wa Ebola katika taifa hilo la Afrika ya kati.