Watu watatu wauawa baada ya gari kugongana na ndovu katika mbuga nchini Uganda

Gari hilo lilikuwa limewabeba wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Uganda.

Newstimehub

Newstimehub

26 Mei, 2026

cf286676161466eb68af0b4d391996a304b791ead44d488ab4fc1715e8164c53

Gari moja limegongana na ndovu katika mbuga ya wanyama nchini Uganda, na kusababisha vifo vya watu watatu na kuwajeruhi wengine wanne, polisi wanasema.

Ajali hiyo ilitokea siku ya Jumapili katika barabara ndani ya Mbuga ya Taifa ya Murchison, polisi waliseama katika taarifa Jumatatu.

Gari hilo lilikuwa limewabeba wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Uganda waliokuwa wamesafiri kutoka mji wa kaskazini kwa Uganda hadi mji mkuu wa Kampala.

Baada ya kumgonga mnyama huyo, dereva “alishindwa kudhibiti gari”, taarifa ya polisi ilisema. “Madereva wanatakiwa kuwa makini sana wakati wanapoendesha kupitia mbuga za taifa na maeneo yenye wanyamapori.”

Video kutoka eneo hilo inaonesha watu waliokuwa ndani ya gari wakiomba msaada huku ndovu ambaye aliyekuwa amejeruhiwa akijikokota kusimama karibu na msitu. Haikufahamika kama ndovu alinusurika katika ajali hiyo.

Pamoja na kuwa matukio haya ni nadra, yanadhihirisha kile wanamazingira wanakitaja kuwa mgogoro kati ya binadamu na wanyamapori ambao unaweza kuibuka katika maeneo ya hifadhi ambayo watu wanatumia.