Zimbabwe inaendelea kuimarisha nafasi yake kama mzalishaji mkuu wa lithium barani Afrika, huku ikirekodi mauzo ya zaidi ya tani 1.13 milioni za lithium concentrate kwenda China mwaka 2025.
Takribani asilimia 15 ya mahitaji ya China ya lithium concentrate yalitoka Zimbabwe, ikionyesha umuhimu wa nchi hiyo katika soko la kimataifa la madini ya betri.
Hata hivyo, serikali inaendelea kushinikiza mabadiliko ya sekta hiyo kwa kuzuia usafirishaji wa madini ghafi na kuhimiza usindikaji wa ndani ili kuongeza mapato ya taifa.
Hatua hiyo pia inalenga kupunguza mianya ya biashara isiyo rasmi na kuongeza uwazi katika sekta ya madini, hasa katika kipindi ambacho mahitaji ya lithium duniani yanaongezeka kutokana na sekta ya magari ya umeme.
CHANZO: Newstimetr














