Liberia inaendelea na mpango wake wa mageuzi ya muda mrefu ya kiuchumi kwa msaada wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) ifikapo mwaka 2027.
Mpango huo pia unajumuisha marekebisho ya kodi katika sekta ya madini na kupunguza misamaha ya kodi ili kuongeza mapato ya ndani kwa ajili ya miradi ya kitaifa kama kilimo, elimu, barabara na usafi wa mazingira.
Benki Kuu ya Liberia imetakiwa kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya mabadiliko ya kiuchumi duniani huku ikiimarisha sekta ya benki na kupunguza mikopo mibovu ili kuchochea mikopo kwa sekta binafsi.
IMF pia imeeleza kuwa mpango mpya utasaidia Liberia kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kujiandaa dhidi ya majanga ya afya ya baadaye.
CHANZO: Newstimetr














