Kisiwa cha Kharg nchini Iran kinachukuliwa kuwa moja ya maeneo muhimu zaidi katika sekta ya mafuta ya nchi hiyo.
Kwa mujibu wa wataalamu wa nishati, kisiwa hicho kinashughulikia takribani asilimia 90 ya mauzo ya mafuta ghafi ya Iran.
Eneo hilo liko takriban kilomita 30 kutoka pwani ya Iran na limekuwa kituo kikuu cha kusafirisha mafuta kwa meli kubwa za mafuta.
Wataalamu wanasema shambulio lolote katika eneo hilo linaweza kuwa na athari kubwa katika soko la mafuta duniani.
CHANZO: Newstimetr














