Serikali ya Uganda imeafikiana na Marekani makubaliano ya kuwapokea na kuwapa hifadhi wahamiaji walionyimwa kuingia Marekani.
Kulingana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Uganda Bagiire Vincent Waiswa, mpango huo utahusisha kuwapokea wahamiaji wenye rekodi za uhalifu, watoto wasio na walezi, na wale wanaosita kurudi makwao.
Waiswa aliongeza kuwa, nchi hizo ziko mbioni kukamilisha mpango na makubaliano hayo.














