Wazima moto wa Morocco waliendelea na juhudi zao Jumapili kuzima moto mkubwa wa msituni katika mkoa wa Chefchaouen kaskazini mwa nchi hiyo.
Afisa kutoka Shirika la Kitaifa la Maji na Misitu la Morocco alisema katika taarifa kwa vyombo vya habari, zilizoripotiwa na vyombo vya habari vya ndani, kwamba moto huo ulianza Alhamisi katika msitu wa Bouhachem katika mkoa huo wakati wa joto kali.
Alisema moto huo umeunguza eneo la takriban hekta 180 za ardhi.
Hakuna majeruhi waliyoripotiwa hadi sasa.