Shughuli za uokoaji zinaendelea katika eneo la Gamo nchini Ethiopia kufuatia maporomoko ya ardhi yaliyosababisha vifo vya zaidi ya watu 100.
Shughuli za uokoaji zinaendelea kusini mwa Ethiopia baada ya maporomoko ya ardhi kusababisha vifo vya watu 102 katika wilaya ya Gacho Baba, eneo la Gamo.
Maporomoko hayo yalitokea baada ya mvua kubwa kunyesha kwa siku kadhaa na kufanya ardhi kuwa laini na hatimaye kuporomoka.
Kwa mujibu wa mamlaka za eneo hilo, miili 52 tayari imepatikana huku juhudi za kutafuta waliopotea zikiendelea.
Msimamizi wa kanda ya Ethiopia Kusini, Tilahun Kebede, amesema serikali imeanza kupeleka mashine nzito kufungua barabara ili kurahisisha shughuli za uokoaji na kupeleka misaada kama chakula, dawa na mahema kwa waathirika.
CHANZO: Newstimetr














