Mvutano umeongezeka katika Mlango-Bahari wa Hormuz baada ya Rais wa Marekani, Donald Trump, kutishia kuchukua hatua kali dhidi ya Iran iwapo njia hiyo haitafunguliwa kikamilifu.
Iran kwa upande wake imesema kuwa haijaufunga mlango huo, lakini imesisitiza kuwa haitaruhusu matumizi ya kawaida kwa meli zinazohusiana na mataifa yanayoishambulia.
Mashambulizi ya kijeshi na majibu ya Iran kwa kutumia makombora na ndege zisizo na rubani yameongeza hofu ya kuongezeka kwa mgogoro, huku athari zake zikionekana kwenye bei ya mafuta na usalama wa biashara ya kimataifa.
CHANZO: Newstimetr














