Umoja wa Afrika wahuzunishwa na ajali ya helikopta iliyoua mawaziri wawili wa Ghana

Kupitia taarifa yake, mwenyekiti huyo alituma salamu zake za rambirambi kwa Rais wa Ghana John Dramani Mahama, serikali ya nchi, watu wa Ghana, pamoja na familia za wafiwa, kufuatia ajali hiyo iliyotokea Agosti 6, 2025.

Newstimehub

Newstimehub

6 Agosti, 2025

3ae7153eab147bfbf54a3b89a8f6b30beb758740278c3a5311cdda79f18f02be

Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Mahmoud Ali Youssouf, amesikitishwa na ajali ya helikopta iliyogharimu maisha ya watu 8, wakiwemo mawaziri wawili nchini Ghana.

Katika taarifa yake iliyotolewa Agosti 6, 2025, Youssouf alisema kuwa amesikitishwa na ajali hiyo, ambayo imechukua uhai wa Waziri wa Ulinzi wa Ghana Edward Omane Boamah na mwenzake wa Sayansi na Teknolojia, Ibrahim Murtala Mohammed.

Kupitia taarifa yake, mwenyekiti huyo alituma salamu zake za rambirambi kwa Rais wa Ghana John Dramani Mahama, serikali ya nchi, watu wa Ghana, pamoja na familia za wafiwa, kufuatia ajali hiyo iliyotokea Agosti 6, 2025.

“Umoja wa Afrika upo pamoja na Ghana katika wakati huu mgumu. Roho za marehemu zipumzike kwa amani.”